Mkali Wenu Aongelea Wimbo wa Alikiba Kubuma
Mchekeshaji wa maigizo ya timamu tv Mkali Wenu amefunguka na kuongelea swala la wimbo wa Alikiba mpya uliotoka hivi karibuni jinsi ulivyotoka lakini hakuna attention yoyote katika mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa katika wimbo wa Seduce me.
Mkali wenu anasema kuwa wimbo wa Seduce me ulikuja na kukatokea vitu vingi sana katika mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na bifu zito kuendelea kati ya Kiba na Diamond lakini huu wa sasa haukuwa na vitu hivyo.
kwakweli kuna tofauti katika alivyotoa wimbo wa seduce me na wimbo wake huu mpya , wakati wa seduce me kulikuwa na vitu vingi sana mara diamond kamwita Ali Kipusa mara vitu vilikuwa vingi sana viliwafanya watu wengine wapate attention ya kusubiri wimbo mpya.baada ya kutoa tu watu wakaona kuwa kidume katoa kitu lakini sasa hivi katoa hakuna skendo yoyote , mange hajaposti kama ilivyokuwa kwa seduce me, imeenda lakini sio kama mzuka wa mwanzoni.