Account Ya Marehemu Godzilla Yadukuliwa na Kugeuzwa Page Ya Umbea

Account ya mtandao wa Instagram ya Aliyekuwa Msanii wa Bongo fleva Godzilla, aliyefariki dunia siku chache zilizopita imedukuliwa.

Ni siku tano zimepita tokea Godzilla apumzishwa kwenye nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kindondoni jijini DSM February 16,2019, lakini jambo lililowahuzunisha wengi ni kitendo cha akaunti yake ya Instagram kua-hacked account na kufanywa page ya umbea.

download latest music    

Msanii wa Hip Hop Fid Q hakutaka kitu hiki kipite hivyo ametumia ukurasa wake wa instagram kutoa taarifa kuwa account aliyokuwa akiitumia Marehemu Godzilla imechukuliwa na sasa inamilikiwa na Umbea Queen na ameonyesha kusikitishwa na kitendo hiko.

Daaah.. Yaani hatujafikisha hata wiki tangu tumpumzishe ndugu yetu kwenye makazi yake ya milele.. HACKERS washapita na page ya insta ya ZIZI..!!? ??”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.