“Afande Sele Ana Stress Zake Anatafuta Pa Kutokea”- Vanessa Mdee

Mwanamuziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee anayefanya vizuri kwenye gemu amefunguka na kudai kuwa msanii mkongwe wa Bongo fleva Afande Sele ana stress zake binafsi ndio maana anatokwa na povu.

Wiki chsche zilizopita Afande Sele akiwa kwenye interview na kituo cha redio alimtaja msanii Vanessa mdee kama msanii anaefanikiwa sio kwa sababu ya kipaji chake au kujua kuimba bali kudai anabebwa na kiki lakini pia anabebwa na penzi lake na msanii Jux. Hii haikuwa mara ta kwanza kwa Afande Sele kumponda Vanessa ameshawahi kumtaja kwenye listi yake ya wasanii wasojua kuimba.

download latest music    

Vanessa alimtolea uvivu Afande Sele kwenye interview aliyofanya na Planet Bongo ya East Africa Radio ambapo alisema kuwa kitendo cha Afande Sele kumponda na kusema kuwa anabebwa alichukulia poa kwa sababu anaelewa Afande Sele alitafuta pa kutokea na stress zake.

Mimi binafsi nilimuelewa niliangalia anazungumzia kwa upande gani nikagundua in few seconds kama nimetumika kama punching bag, sikuchukulia personal, nikaona fresh kabisa, nikajua anhaa alikuwa na yeye anataka kusikika anatafuta pa kutokea kihivyo ila mimi ni shabiki yake Mkubwa akawa ameniua kihivyo yaani amenitathimini kaniona hivyo ila kiukweli yule ni legend pia”.

Lakini pia Vanessa amesema kuwa anaelewa kuwa Afande Sele ni mkongwe kwenye game ila huenda alikuwa na stress zake binafsi, hivyo alikuwa anatafuta pa kumalizia hasira zake ndipo alipoangukia kwa Vanessa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.