Ali Kiba Aibuka Kidedea Tena Amgaragaza Diamond na Wasanii Wengine Kibao

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Ali Kiba ameibuka kidedea kwa kutajwa kama msanii mwenyewe ushawishi mkubwa Tanzania.

Tuzo hizo zinazojulikana kama 100 Most Influential Youth zilizoandaliwa na Advance Media organization zilitangazwa rasmi mwaka Jana na mastaa kibao walitajwa kuwania tuzo hizo.

download latest music    

Baadhi ya Mastaa walioshindanishwa katika tuzo hizo ni pamoja na Alikiba, Jokate, Vanessa Mdee, Diamond Platnumz, Wema Sepetu, Idris Sultan, Faraja Nyalandu, Nancy Sumari, Dina Marios, Millard Ayo na wengineo wengi.

Siku ya Jana ilitangazwa rasmi kuwa Ali Kiba amembwaga hasimu wake namba moja Diamond baada ya kutajwa kuwa ndio msanii mwenye ushawishi Mkubwa sana na kupewa medani ya sanaa na burudani katika tuzo za advance media 2017/2018.

Matokeo ya kura zilizokuwa zikipigwa za 50 Most Influential Tanzanians (vijana 50 wenye Ushawishi zaidi) yametoka na katika kipengele cha burudani (Entertainment) Mshindi ni Ali Kiba huku akimshinda hasimu wake Mkubwa Diamond ambaye yeye amechukua nafasi ya pili , akifuatiwanam Wema Sepetu aliyechukua nafasi ya tatu huku nafasi ya nne imechukuliwa na mchekeshaji Joti na nafasi ya tano imechukuliwa na Vanessa mdee huku Jokate Mwegelo akichukua nafasi ya sita .

Baada ya ushindi huo Ali Kiba alitumia ukurasa wake wa Instagram kuandika salamu zake za shukrani kwa mashabiki zake baada ya kumpigia kura:

 

Thank you for voting for me to become the most influential Young Tanzanian in Entertainment Industry Nawashukuru sana #Kingkiba”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.