Ali Kiba Awatupia Dongo Wasanii Wanaonunua ‘Views’ Youtube

Mwanamuziki wa Bongo fleva Ali Kiba anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Mvumo wa radi’ amedai kuwa kuna wasanii wenzake ambao wana tabia ya kununua viewers (watazamaji) Youtube.

Ali Kiba alipatwa na sakata hilo la views huko Youtube baada ya video yake kuanza kupoteza watazamaji badala ya kuongezeka kitu kilichodaiwa kuwa ni figisu figisu tu alizofanyiwa na watu.

download latest music    

Kwenye Interview aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Ali Kiba alikiri wazi wazi kabisa kuna wasanii ambao wana tabia ya kununua views Youtube ilimradi tu wavunje rekodi jambo ambalo hawezi kufanya maana ni utoto:

Tunajua kabisa kuna hizi bisness za kuweka maroboti katika hizi YouTube, watu wanajifanya wana views wengi na nini. Hivi vitu vipo, tena vipo!, vipo sana tu!, vipo tena sana boss!

Eeeh, wananunua lakini kwa mimi binafsi naona ni utoto, mimi nafanya muziki wangu kwa ajili ya watu, kwanini nidanganye watu“.

Lakini pia Ali Kiba amepasua kuwa hizo views za Youtube hazimsumbui sana kwani ana njia zake nyingine za kumpatia pesa Kwenye muziki na sio Youtube tu.

Haijaathiri chochote, watu wamepata walichokuwa wanataka na sio mimi nategemea pesa kutoka YouTube viwership, hapana!. Ninachotaka kwangu ni mashabiki wangu waridhike waelewe kabisa wana-deal na msanii wa aina gani“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.