Ali Kiba Azidi Kupaa na Kuenda Level Nyingine

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva anayefanya vizuri na wimbo wake wa ‘seduce me’ Ali Kiba amezidi kukaa juu zaidi kwenye chati hasa mwaka huu wa 2018 unaonekana utakuwa mwaka mzuri kwa Ali Kiba.

Ali Kiba ni moja ya wasanii Bongo fleva ambaye ni msiri sana katika mambo yake binafsi watu wengi wanafahamu kuhusu kazi zake binafsi lakini ni ngumu sana kujua nini kinaendelea katika maisha yake binafsi au hata katika kazi zake binafsi.

download latest music    

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi kuwa Ali Kiba anakuja na bidhaa zake sokoni ambapo ilisemekana anaweza akawa mmiliki au balozi wa bidhaa kadhaa lakini hakuna siku ambayo Ali Kiba aliweza kuthibitisha taarifa hizo.

Lakini huu mwaka ni lazima utakuwa mwaka wa Ali Kiba kutengeneza pesa ingawa anafanya mambo kimya kimya kwa sasa lakini kuna video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii iliyoonyesha Energy drink inayoitwa ‘Mo Faya’ ambayo ilikuwa na jina la  Alikiba na Sura ya Alikiba.

Lakini Mpaka sasa haijawekwa wazi kama yeye ni mmiliki wa kinywaji hiko au ni balozi wa kinywaji hiko lakini kitu ambacho kinajulikana na ukweli juu yake kutoka katika mtandao wa Dizzim Online ni kuwa mmiliki wa kinywaji hiko anaitwa Dj Sbu ambaye ni mkazi wa South Africa ambaye ameonekana mara kadhaa na Ali Kiba. Ali kiba ataungana na ulimwengu wa wasanii wafanyabiashara kama Diamond, Vanessa na Jux.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.