Alichofanya Diamond ni Heshima kwa Wasanii Wengine :-Steve Nyerere.

Msanii a vichekesho nchini Steve nyerere amefunguka na kusema kuwa pamoja na kwamba watu watakaa wakibeza kile alichofanya Diamond lakini ukweli utabaki kuwa alichofanyadiamond ni heshima kuwa kwa wasanii na kazi ya sanaa pia kuwa kuwa wasanii wanaweza kufanya kitu katika jamii.

Steve nyerere ambae amekuwa akiponda au kusifia bila kuogopa pale msanii anapokosea au kufanya vizuri  amesema kuwa kitu alichofanya Diamond inabidi kiwe mfano wa kuigwa hata kama  haitawezekana kufanya kwa kiwango chake.

download latest music    

Steve anasema “Huwezi kuzuia ukweli upite; Tumekuwa watu wakubisha bila sababu, Niambiwe ni 
nani alishawahi kujua waliomfanya awe wanaitaji msaada wake.Alicho kifanya Diamond ni HESHIMA kwa wasanii wengine, amefanya kwa Niaba ya Sisi WOTE.

Kama kuna MTU anabeza atakuwa DODOKI, Diamond ni mfano wa kuigwa, Kuna Watu walikuwa maarufu kuliko Diamond Ila waliishia sifa YA kujitapa mtaani na kudharau watu, MIMI KWANGU NAOMBA TUKUMBUKE TULIPO TOKA.Sanaaa ni KAZI, IFIKE Muda tujue ADUI wa sanaa ni Sisi wenyewe. Daimond songa umefungua milango ya huduma kwa JAMII KAKA

Hata hivyo steve nyerere amehaidi na kusema kuwa hata yeye atakuja kufanya vitu vikubwa sana zaidi ya alichofanya diamond kwa jamii yake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.