Alichofanya Hamisa Ni Zaidi Ya Ubinadamu

Ni wengi tunaonekana kuwa na furaha tena hasa pale ambapo unaoona kama  mtu uliyekuwa haulewani nae au upo nae katika ugomvi kwa muda mrefu anapata matatizo na kuumia.Pengine miaka miwili ni mingi sana kwa Lulu kuona haya ambayo wasanii wenzie wameyaandika juu yake lakini pia Mungu ndie anaepanga kila kitu inawezekana pia ikawa ni bahati na akaweza kuyaona majonzi ya watu walikuwa wakimlilia hivi karibuni.

Hamisa alikuwa ni moja ya watu ambao hawakuwa katika maelewano mazuri na Lulu  kwa muda mrefu kidogo kama miaka miwili hivi, kwanza kabisa ni kutokana na msanii Lulu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na baba mzazi wa mtoto wa kwanza wa kike wa Hamisa, lakini pia hivi karibuni lilipotokea sakata la Hamisa na Diamond kuhusu mtoto wake wa pili ,Lulu  alionekana kwa kiasi fulani kuwa upande wa Zari.

download latest music    

Lakini yote hayo hayakumfanya Hamisa jana kuonyesha hisia zake za kuumia baada ya Lulu kupata hukumu ya kifungo cha miaka miwili jela.Pamoja na yote bado Hamisa alitambua mchango mkubwa aliokuwa nao Lulu kwa mtoto wake Fantancy ambae alizoea kumwita aunty kutokana na uhusiano wa karibu wa Lulu na baba wa mtoto huyo,

Ukiachana na post aliyoweka instagram, lakini pia Hamisa alifanya interview jana na televisheni ya Clouds plus, na hakusita kuelezea maumivu yake kwa kile kilichomkuta Lulu. Na kusema kuwa bado hakuwahi kumuona Lulu kama mtu mbaya kwa sababu alikuwa ni mama mzuri kwa mwanae.

Namjua Lulu, naujua upande wa mama Kanumba na upande wa Lulu pia, lakini ukirudisha  nyuma two years ago mimi na Lulu tulikuwa na mambo fulani, everybody knows sio mpaka niyaseme,na inapofika kwenye jambo ambalo ni tatizo its not good, na unajua watanzania  hata ukifanya kitu kwa nia nzuri, as much as i would love to kwa sababu mwisho wa siku  she is not a bad person kwangu especially kwa mwanangu , she has been a very good aunty, ni mtu ambae nilikuwa naweza kumuamini kwamba akiwa na mwanagu yuko safe ingawa nilikuwa najua ni mwanamke mwingine wa baba yake lakini nilikuwa najua yuko stable.-   Alifunguka Hamisa Mobeto.

Lulu alikiuwa na uhusiano wa kimapenzi na mzazi mwenzie na hmaisa mobeto na hata mara nyingine mtoto huyo alikuwa akikaa kwa lulu kama kwa mama na alikuwa akimtunza vizuri kwa mujibu wa Hamisa mwenyewe.

Hamisa akiwa na mwanae  Fantancy, mtoto aliezoea kumwita Lulu aunty

Lulu akiwa  Majizzzo ambae pia ni  mzazi mwenzie na Hamisa Mobeto.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.