Alichokiandika Ommy Dimpoz Katika Siku Yake ya Kuzaliwa.

Ikiwa leo ni 13 septemba , ni siku ya kumbukumbu ya watu wengi lakini pia ni kumbukumbu ya kuzaliwa ya msanii Ommy Dimpoz na aliamua kuweka picha yake aliyowahi kupigwa kipinid akiwa mgonjwa sana na akiwa katika chumba cha wagonjwa mahutiuti siku za nyuma.

Ommy dimpoz amweka picha hiyo na kuandika maneno yenye hisia sana huku akijaribu kumshukuru Mungu na watu wote kwa ujumla ambao wamekuwa nae kwa kipindi chote cha ugonjwa wake na maobi waliokuwa wakituma kwa mwenyezi mungu kwa ajili ya afya yake.

download latest music    

Ommy anasema kuwa haikuwa rahisi yeye kuwa katika hali ile lakini leo yuko mzima na  anaweza kurudi katika hali yake kama kawaida , lakini pia anwakumbusha watu kuwa ugonjwa ni ibada ambayo mungu anaamua kukupitisha ili kukukumbusha kuwa yeye yupo.

Ommy anasema kuwa kuna kipindi alikuwa tayari ameshakata tamaa kabisa ya kuishi , lakini alipokuja mgonjwa mwingine ambae alikuwa ameshambuliwa na majambazi na madaktari wakamtibu na kuokoa maisha yake ndipo alipoamini kuwa hata yeye mungu atampigania kwa sababu mungu ndie mwenye nguvu pekee yeye  haja haja ya kukata tamaa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.