Alichosema Chuchu Hans kuhusu ndoa yake.

Msanii wa Bongo Movie Chuchu Hans amefunguka na kuongelea swala la ndoa yake na msanii mwenzie vicent Kigosi maarufu kama Ray , wawili hao wamekuwa katika mahusiano zaid ya miaka mitatu sasa na ni miezi kama minane tu imepita tangu Chuchu  ajifungue mtoto wao wa  kiume anayeitwa Brian.Hata hivyo msanii huyo wa kike alipokuwa akihojiwa aliongelea swala la yeye kufunga ndoa na baba mzazi wa mtot wake huyo.

Alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa tetesi za yeye kuolewa na ray kabla ya kubeba mimba ziliishiwa wapi alijibu kuwa ni kweli  lakini mipango iyo kwa sasa haipo tena,na alipoulizwa sababu kubwa ya yeye kutaka kuhaishirisha jambo ilo Chuchu anasema kuwa inawezekana kwa sababu yeye na baba wa mtoto wake wamezoeana sasa ivyo kwakwe ni kawaida ila hakuna sababu yoyote ya yeye kukataa kuolewa nae.

download latest music    

Kuhusu maisha yake ya ulezi na mtoto wake  mrembo huyo alisema kuwa kwa sasa wanaendelea vizuri na maisha ya ulezi na baba wa mtoto anafanya majukumu yake kama baba na yeye pia anafanya majukumu yake kama mama mzazi.Kwa mujibu wa Chuchu  mahusiano yao yanaendelea vizuri na ndio maana aliamua kumpa baba mzazi huyo zawadi ya mtoto, kwa sababu umri pia unakwenda ivyo ni wakati sahihi yeye kumzawadia mpenzi wake huyo.

Hata hivyo Chuchu  Hans anasema kuwa kwa sasa hivi bado hajafikiria bado kuongeza mtoto wa pili, na kuhusu kumuonyesha mtoto wao wa kiume sura ambae mpaka sasa mtoto huyo ana miezi nane lakini bado hawajaamua kumuonyesha katika mitandao, amesema kuwa huo ni uamuzi wa baba wa mtoto.

Chuchu  Hans ni moja kati ya mastaa wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu,, ukiachana na kuzaa na Ray mtoto mmoja Chuchu tayari alikuwa na watoto wawili  kabla ya kukutana na baba mzazi wa mtoto wake huyu mdogo. Lakini kwa sasa amejikita katika tasnia ya filamu na wanakampuni  yao  ambayo inasimamiwa na yeye mwenyewe.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.