Alichosema Mama Kanumba Kuhusu Lulu.

Mama wa marehemu Steven Kanumba amefunguka na kusisitiza kuwa katika maisha yake hajawahi kumchukia msanii Lulu Michael kama ambavyo imekuwa ikisikika masikitonkwa watu na watu wengi kuamini hivyo kwa sababu ya kumuua mtoto wake.

Mama huyo anasema kuwa hajawahi kumchukia Lulu lakini amekuwa na uchungu kila siku kwa sababu kifo chake kimesababishwa na mtu mwingine.

download latest music    

Mama kanumba alipokuwa akiongea na EATV, anasema  “kanumba ni mwanangu na nilikuwa ninampenda sana na ukizngatia nilimlea kwa tabu sana lakini anatokea mtu anamuua, mimi simchukuii lulu mimi ninampenda sana, ninamtakia kila lenye kheri katika maisha yake.

Kama bado kuna kumbukumbu, mama kanumba na lulu walikuwa marafiki sana hasa baada ya kifo cha kanumba lakini baada ya hapo mahusiano yao yalianza kufa na hata kufikia hatua ya kuwa maadui wakubwa.

Mama huyo ukiachana na kulalamika  katika mitandaokuwa lulu amekuwa hamuheshimu wala kumsaidia lakinni alichukizwa sana na hukumu aliyopewa mwanadada huyo ikiwa kama adhabu ya kifo cha msanii huyo ambae alikuwa katika mahusiano  na Kanumba.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.