Alikiba adhihirisha yeye ni rafiki wa dhati na gavana wa Mombasa Hassan Joho

Alikiba amekua kando ya Hassan Joho mbaka wakati wa mwisho ambapo gavana huyo wa Mombasa alishinda kura na kuteuliwa kwa kipindi cha pili kama gavana.

Alikiba alisafiri kuelekea Kenya kumpigia debe Hassan Joho katika harakati zake za kutafuta kura katika jimbo la Mombasa. Staa huyo wa Bongo Flava ata alitunga wimbo kumsifu gavana huyo.

download latest music    

Kiba pia alitumbuiza Wakenya katika kampeni ya mwisho ya mrengo wa Nasa iliyofanyika Nairobi wikendi ya mwisho kabla ya Wakenya kupiga kura.

Alikiba, Hassan Joho na Raila Odinga wakiwa kwenye jukwa jijini Nairobi

Baada ya kufanya kampeni Nairobi, Staa huyo alirejea Mombasa na gavana Joho na alikaa na yeye mbaka vile uchaguzi ukaisha.

Alikiba alionekana akimsindikiza gavana huyo kwa kituo cha kuhesabu kura ambalo lipo Bandari College jijini Mombasa.

Ali Kiba na Joho wakiwasili kwenye kituo cha kuhesabu kura jijini Mombasa

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere