Alikiba amtetea Chid Benz

Alikiba amepinga shinikozo za kufungwa kwa msanii Chid Benz ambaye alikamatwa na dawa ya kulevya ya aina ya heroin.

Akiongea na eNews ya EATV, Kiba alimtetea Chid Benz kwa kusema kuwa anapofungwa mtumiaji wa dawa za kulevya ni kumtesa bali anapaswa kupelekwa katika vituo vya afya ili aweze kupatiwa tiba mbadala.

download latest music    
Chid Benz

“Unapomfunga mtu ambaye ni mtumiaji wa dawa za kulevya ni mateso makubwa kwa kuwa mtu huyo anapaswa apelekwe kitengo maalum ili apatiwe dawa za kuzuia kutamani vitu vya aina hivyo, pia yeye mwenyewe tunapaswa tumshauri ili aweze kushinda nafsi yake. Ujue vitu kama hivyo ni kuishinda tu nafsi katika kuamua na akae navyo mbali. Kama ametoka ‘Rehab’ hivi karibuni halafu inasemekana amejihusisha tena na hivyo vitu ni makosa makubwa kwa sababu tayari umetoka katika kupata tiba halafu unayakaribia tena hiyo haifai kabisa,” alisema Alikiba.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere