Aliyoyasema Baba Diamond Kuhusu Mimba ya Tunda

Baba mzazi wa msanii Diamond amefunguka na kuolengea mambo yanayoendelea katika mitandoa ya kijamii kuhusu mtoto wake huyo na mahusiano mapya ya kimapenzi yanayosemekana kuwepo katika yake na video queen maarufu bongo Tunda na kwamba mrembo huo saa hivi ni mjamzito na mimba  ni ya Diamond.

Baba huyo amesema kuwa kwa pande wake hana kinyongo chochote kuhusu mimba hiyo na kama yeye mwenyewe amekubali basi yeye hana shida kwa sababu binadamu hakataliwi hata siku moja.Hata hivyo baba huyo anasema kuwa hamjui kabisa mwanamke anaeitwa Tunda kwa sababu hata yeye hafatilii sana mitandoa ya kijamii.

download latest music    

Sijui habari zozte kuhusu Tunda, maana sio mtu wa kufutailia katika mitandao lakini watu ninaowajua alishawahi kutembea nao ni Wema Sepetu, Zari na Mobeto.Huyo Tunda simjui kabisa lakini kama itakuwa kweli yeye mwenyewe karidhika basi haina shida mimi sitakaa kuitwa babu ukubwa jalala.uwezi kukataa mtoto wa mtoto wako.

Hata hivyo Baba Diamond amesema kuwa ameona katika gazeti kuwa mtoto wake huyo kapanga nyumba , lakini hajafatilia kwa sababu ameona tu katika magazeti na hawezi kusema kama habari hizo zina ukweli au la.

Kuhusu swala la ,Mama Diamond kuolewa na mwanaume mwingine mzee huyo amesema kuwa yeye na Sandra kwa sasa ni kama dada na kaka na wamekuwa marafiki tu wamekuwa wakikutana nakusaidia ushauri kimaisha  lakini hawezi kumonea wivu kwa kuolewa kwa sababu walishaachana siki nyingi sana. Na kama ni kweli kuwa mama huyo ameolewa na ni mjamizto basi ni jambo la kheri na ana muombea dua ili aweze kufankiwa katika hilo lakini hana wivu kabisa.

Ilo la kusema kaolewa mimi wala sijakasirika kwa sabau tulishaachana siku nyingi sana,ingawa watu wanakuwa wanasema namuachia yeye anapanda ndege, ninachiamini mimi ni kuwa ndege yangu ipo na kuna siku nitaipanda tu.kikubwa tu ninamuombea mungu aweze kufanikisha katika ndoa yake na kama ni kweli kuwa ana mimba basi ninamuombea dua kwa hilo.-Alisema baba yake mzazi na Diamond.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.