“Ati Madale State Lodge, au Madale State House?” Zari Aendelea kumpiga Madongo Diamond

Mfanyabiashara maarufu Zarinah Hassan ‘Zari’ ambaye pia ni mpenzi na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amejikuta anashindwa kuvumilia kinachoendelea mtandaoni na kumtupia madongo mpenzi wake.

Tangu wiki hii inaanza stori iliyotawala mitandao ya kijamii ni uhusiano uliopo baina ya Diamond na mrembo Tunda. Tangu mwanzo wa wiki kilichokuwepo ni tetesi tu na maneno ya watu yaliosemwa mpaka Jana video iliyosambaa mtandaoni ilitomuonyesha mdogo wa Tunda akijiachia Nyumbani kwa Diamond Madale.

download latest music    

Ifahamike kuwa nyumba ya Diamond iliyopo maeneo ya Madale ilibatizwa jina la ‘State house’ ikimaanisha mjengo wa raisi/ Ikulu na Guest House ikimaanisha nyumba ya kufikia wageni.

Baada ya stori ya Jana kutoka kuwa msichana huyo amejirekodi akitembea Madale lakini pia Hamisa na yeye ameshajirekodi akiwa Madame inaelekea uzalendo ulimshinda Zari ikabidi amrushie dongo hill la kuhoji endapo  nyumba hiyo bado ni jumba la raisi au imekuwa ni guest house?

Zari alihoji hayo kupitia ukurasa wake wa Snapchat na kuandika:

Ati Madale state lodge or Madale state house? Kuna mtu alikuwa anauliza akipanda Bajaji anashukia wapi? Mama yangu sio state house Tena….”.

 

Tetesi za Diamond kutembea na Tunda zimekuwa zikisikika mjini hapa kwa muda mrefu lakini wote wawili wamekuwa wakizikana lakini pia hivi sasa kuna habari zinazodai kuwa Tunda ni mjamzito na Diamond ndiye baba mtoto ingawa ni taarifa tu ambazo hazijathibitishwa na Tunda wala Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.