Aunty Ezekiel- Sipendi Kuishi Maisha Ya Kuigiza Mitandaoni

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Aunty Ezekiel amefunguka na kuweka wazi kuwa hawezi kuishi maisha ya kuigiza tajiri kwenye mitandao ya kijamii wakati hana kitu.

Aunty amefunguka hayo baada ya hivi karibuni kusemwa Kwenye social media baada ya kuonekana amerudia nguo aliyovaa Kwenye msiba wa mtoto wa  Muna ambayo alishavaa Kwenye misiba kadhaa siku za nyuma.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Amani, Aunty Ezekiel, amesema anawashangaa watu wanaomjadili kuwa anarudia nguo na kumtaka anunue nguo kila siku kitu ambacho yeye anaona hakina maana.

Eti kila sehemu niende na nguo mpya au hata msibani nibadili nguo ina maana nitakuwa sina vitu vingine vya kufanya vya maendeleo zaidi ya kununua nguo kwa ajili ya maonyesho? Watu wasinijadili, sina muda huo wala kufuata wanayotaka wao”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.