Aunty Lulu Aunga Mkono Operesheni Ya Makonda

Msanii wa filamu za Bongo movie Lulu Semagongo maarufu Kama Aunty Lulu ameibuka na kudai anaunga mkono jitihada za mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda za kupambana na Mashoga.

Wiki mbili zilizopita Mheshimiwa Paul Makonda alitangaza rasmi vita na Vijana wanaofanya Mapenzi ya jinsia moja maarufu Kama Mashoga katika mkoa wa Dar Es Salaam.

download latest music    

Katika mahojiano yake na Global Publishers, Aunty Lulu amedai amefurahishwa mno na hatua aliyoichukua Makonda kwani naye ni mmoja wa mastaa waliokuwa wakiishi na mashoga, lakini Mungu akamuokoa na kuachana nao hivyo zoezi hilo litasaidia kwani mashoga hao wamesababisha hata wanawake wasiolewe.

Ninampongeza sana Makonda maana hawa mashoga ni janga la kitaifa, naomba akishawakamata wakipimwa na kugundulika wanafanya ufuska huo, wakusanywe kwenye uwanja mkubwa wachapwe viboko baada ya hapo ndiyo wapelekwe gerezani kwa sababu wanawake tunakosa kuingia kwenye ndoa kwa sababu yao”.

Lakini pia Aunty Lulu alimuomba Makonda azungumze na Rais John Pombe Magufuli ili msako ufanyike kwa nchi nzima kwani mashoga wengi wamekimbia jijini Dar na kwenda mikoani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.