Baada Ya Shilole Kuolewa Jana Nuh Mziwanda Adai Alilala na Shilole Siku Chache Zilizopita

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda amefunguka na kudai kuwa alilala na bibi harusi ambaye ni Shilole wiki moja kabla ya harusi.

Wiki iliyopita kuna picha zilienea mtandaoni zilizomuonyesha Shilole akiwa amelala kimahaba kabisa kitandani na aliyekuwa mpenzi wake hapo nyuma Nuh Mziwanda na zikasindikizwa na habari kuwa wawili ha wamerudiana jambo ambalo Shilole alilikataa haraka sana huku akidai picha zile zilikuwa za siku nyingi na akadai aliyesambaza picha zile alikuwa ni Nuh Mziwanda ili tu amharibie uhusiano wake na mchumba wake Uchebe.

download latest music    

Picha hizo zilionekana ni za hivi karibuni kwa sababu ya tatoo aliokuwa nayo Shilole ilikuwa ni mpya lakini pia nywele alizosuka pia zilikuwa ni za hivi karibuni. Lakini cha ajabu mpenzi wa Shilole Uchebe alipohojiwa alikiri kuwa Shilole alichepuka na Nuh Mziwanda wiki iliyopita lakini kwa sababu anampenda ameamua kumsamehe tu .

Siku ya jana usiku Shilole na Uchebe walifunga ndoa ghafla ghafla huku ikihudhuriwa na watu kumi na tano tu ambao ni familia ya maharusi na mt pekee maarufu aliyekuwepo ni Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond ambaye alisimama pale kama mzazi wa Shilole ambaye alisaidia mpaka kufanikiwa katika ndoa ile ya kimya kimya.

Lkini katika hali ya kushangaza Nuh Mziwanda ameonyesha kutfurahishwa na ndoa hiyo ya ghafla kwani kupitia ukurasa wake wa Instagram amefunguka na kuadika ujumbe wa mafumbo na  i kama kijembe kwa Shilole na Uchebe na ujumbe huo unasomeka kama ifuatavyo:

Aliye Lala na bibi harusi wiki moja kabla ya harusi na wala sio bwana harusi bado mnanshauri harusi? (All girls are pretenders)”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.