Baba Diamond Adaiwa Kukaata Mtoto Wake Wa Nje

Baba mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma ametupiwa tuhuma nzito baada ya kudaiwa kutelekeza mtoto wake wa nje.

Global Publishers wanaripoti kuwa kijana aliyejitambulisha kwa Jina la Emmanuel alidai ni mtoto wa Baba Diamond na ametoka mkoani Kigoma kwa ajili ya kuja kuonana na Baba yake ambaye mama yake amemwambia alimtelekeza.

download latest music    

Gazeti hilo lilimsaka Baba Diamond ili kujua ukweli wa tuhuma hizo ambapo alikiri kumpokea kijana huyo na kusema kwamba siyo mtoto wake kama mwenyewe anavyodai bali ni kijana tu ambaye alikuwa anatafuta njia ya kukutana na Diamond kwa hiyo akaona njia rahisi ya kumfikia ni kujifanya mtoto wake.

Nilikuwa katika pilikapilika zangu, mara nikapigiwa simu nikaambiwa kuwa kuna mgeni wangu nyumbani, nilipouliza ni nani nikaambiwa ni ndugu yake Diamond ambaye ni muimbaji pia katokea Kigoma.

Baada ya kumaliza pilika zangu nilirudi nyumbani na kweli nikamkuta kijana huyo lakini cha kushangaza alikuwa anatetereka sana kujibu maswali kwa sababu hata nilipomuuliza jina la baba yake alitaja lingine kabisa tofauti na langu.

Unajua huyu siyo kijana wa kwanza kuja na kudai kuwa mimi ni baba yao, wanatafutaga njia ya kutaka kuonana na Diamond lakini wanashindwa kutokana na mama yake kule ni mkali hawawezi kuingia, kwa hiyo wanataka waje kwangu kwa sababu wanajua nafika kwa Diamond.

Wanahisi wakidanganya hivyo itakuwa rahisi mimi kuwakutanisha kitu ambacho hakiwezekani, narudia tena mimi sina mtoto wa nje kwa sababu watoto wangu wote nawafahamu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.