Baba Diamond Amshauri Zari Amvumilie Diamond Kwa Mapungufu yake

Baba mzazi wa Mwanamuziki Diamond Platnumz Mzee Abdul ameibuka na kumshauri Zari aendelee tu kumvumilia Diamond kwa makosa aliyoyafanya.

Katika mahojiano aliyoyafanya na Mllard Ayo Baba Diamond alipoulizwa akikutana na Zari atamshauri nini kuhusu mtoto wake ndipo aliposema kuwa atamshauri awe mvumilivu.

download latest music    

Baba Diamond amesema;

“Kwanza awe mvumilivu kwani mtoto wa kiume anakua mtu wa kudanganywa, mpotofu na ilimradi kashaambiwa kuna mke mwenzie basi awe mvumilivu ila kikubwa tu kuwe na heshima na adabu Zari kama Zari na Hamisa kama Hamisa waheshimiane wawe pamoja waangalie maisha tu yanaenda kama kawaida”.

Pia Mzee Abdul aliendelea kusema:

“Zari mi namwambia asipende kuwasikiliza waswahili ilimradi aangalie yake yanamwendea vizuri na Hamisa naye asipende kusikiliza ya Waswahili akae aangalie yake aendelee vizuri maana sisi waswahili kila neno linakuwa baya kwetu hamna neno zuri na mara nyingi tunakuwa hatupendani kupendeana mema mtu anapenda mwengine haaribikiwe asemwe tu, ila wakae pamoja tu waangalie haya maisha leo tupo kesho hatupo”.

Baba Diamond pia alimuomba Zari kama kuna uwezekano basi apewe nafasi awaone wajukuu zake akimaanisha Latiffah na Nilllan ambao amekiri hajawahi kuwaona kutokana na kutokuwa na  uhusiano mbovu na mtoto wake Diamond.

Baba Diamond aliongeza;

“Mi napenda kumwambia Zari nikiwa mimi kama mimi Baba Diamond aniletee wajukuu zangu kwanza niwaone au sio lazima nianiletee anaweza hata akaniambia sehemu gani naweza niweze kuenda kuwaona wajukuu zangu”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.