Baba Diamond- Natamani Diamond Angenialika Tandale

Baba mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma maarufu kama Baba Diamond ameibuka na kudai mwanaye hakumualika kujumuika naye Tandale wiki iliyopita.

Wiki iliyopita Diamond aliongozana na Familia yake yote akiwemo mama Yake na dada zake pamoja na Familia nzima ya WCB katika charity event aliyofanya maeneo ya Tandale Maguniani.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Baba Diamond amefunguka na kusema anatamani angekuwepo kama sehemu ya kukumbuka maisha yao waliyoyapitia miaka ya nyuma akiwa na mwanaye huyo kwani historia aliyoitoa Diamond ilimgusa.

I wish na mimi ningekuwepo pale. Nilitamani kushuhudia pia mambo mazuri aliyoyafanya mwanangu maana awali nilidhani ni jambo dogo, lakini baadaye nikaona ni jambo kubwa sana.

Nilipofuatilia kwenye TV nikaona mwanangu anatoa Bajaj, anatoa bima, anatoa mikopo kwa akina mama, pamoja na bodaboda kwa kweli moyo wangu ulifurahi sana.

Ile ishu ya kuuza mitumba aliyoizungumza, hata mimi niliuza. Pengine pia ningeweza na mimi kuwatia moyo mamia ya watu waliofurika pale.

Nilisikia alisema amepanga kufanya kila mwaka hivyo bado naamini Mungu akitujalia uzima, ishallah mwakani anaweza kunialika kwani hakuna tatizo kati yetu”.

Diamond amekuwa hana Mahusiano mazuri na Baba yake kwa miaka mingi hii ilitokana na Baba Diamond kumtelekeza Diamond wakati mdogo na hivyo kulelewa na mama yake ambaye yupo naye karibu zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.