Baba Kanumba Hakuridhika Na Hukumu Ya Lulu

Wakati watu wengine wakilalamika na wazazi wa msanii Lulu Michael hata kuzimia na kushindwa kutembea kutokana na hukumu aliopewa msanii Lulu Michael ya kutumikia kifungo kwa miaka miwili jela baada ya kukutwa na hatia ya kumuua marehemu Steven Kanumba bila kukusudia , baba mzazi wa marehemu Kanumba amefunguka na kusema kuwa hukumu hiyo iliyotolewa na mahakama ni sawa na mtu alieua kuku tu.

Akiongea kwa njia ya simu moja kwa moja kutoka mkoani Shinyanga anapoishi mzee huyo na mwandishi wa Global publisher, baba Kanumba aliulizwa anasemaje maoni yake kuhusu hukumu aliyopewa Lulu baaada ya kukutwa na hatia ya kumuua mwanae bila kukusudia na alijibu kuwa

download latest music    

Kwa upande wangu kwanini  hukumu hii imekuwa  ndogo sana, na haijanifurahisha hata kidogo, hata kama mtu aliua kwa kutokukusudia  lakini mahakama imetoa kifungo cha miaka miwili kweli kama mtu kaua kuku.-Alifunguka mzazi huyo

Hata hivyo alipoulizwa kama angefurahi ni miaka mingapi ambayo alitegemea Lulu angepewa mzazi huyo alisema kuwa,

nilitegemea kuwa mahakama ingetoa hata kuanzia miaka mitano,sita,saba na kuendelea.

Hata hiVyo kuhusu yeye kutokuwa anaonekana mahakamani, baba mzazi wa Kanumba alisema kuwa alishindwa kuja ili kukwepa gharama na ndio maana alimuachia mama yake aweze kufatilia swala hilo hata hivyo anaona ingekuwa ni upotevu wa pesa maana hata hiyo hukumu yenyewe sio ya msingi sana.

Sikuja huku nilimwachia mke wangu aendelee na kesi  hiyo kutokana na kupunguza  sizizo na msing na ndo hivyo hukumu yenyewe  ni miaka miwili tu kama mtu kaua kuku.si ningepoteza muda wangu tu hapo na hukumu yenyewe haikunifurahisha  kulingana na mazingira ya kifo cha mtoto wangu .-Aliongezea Baba Kanumba

Lulu Michael alimuua Kanumba bila kukusudia miaka kama mitano iliyopita na baada ya kesi yake kushughulikiwa kwa muda mrefu ameweza kuukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kitu ambacho kiliibua pia hisia za watu wengi wanaompenda Lulu na  watu wengi kuonekana na majonzi kutokana na hukumu hiyo huku kila mmoja akiibua lake.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.