‘Baba’ ya mtoto wa Hamisa Mobetto ajitokeza

Dennis Louis ambaye ni mshindi wa milioni 50 za Tanzania Movie Talent amejitokeza kudai kuwa mtoto wa Hamisa Mobetto ni wake kupitia mtandao wake wa Instagram.

Muigizaji huyo alianzak kwa kusema kuwa Diamond Platnumz sio baba ya mtoto yule bali yeye ndio baba wa halali. Dennis Louis aliweka post hiyo huku akiwaacha wengi kama wameshangaa. Aliandika;

download latest music    

“Mengi yamesemwa nimevumilia vya kutosha mwenye mzigo nadhani mshanijua!! Kabla hamjaandika mambo zenu muwe na evidence za kutosha!!. Basi wenye wivu watasema Photoshop shubaaamit!!! #babajunior #comingsoon”

Hata hivyo hakuwachia hapo kwani aliweka post nyingine yenye picha yake na Hamisa Mobetto ameandika,

“son you have a bright future behind you…#eyoo! It’s a boy”

Mashabiki nao ambao wamekuwa wakifuatilia akaunti za Hamisa na Tanzanian baby walimshambulia huku wakisema kuwa wanajua kuwa msanii huyo anatafuta Kiki.

Kufikia Sasa Hamisa bado hajaweka wazi mtoto wake huyo wala baba ya mtoto wake.

 

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua