Babu Tale Afungukia Matibabu Ya Hawa Nchini India na Ugonjwa Unaomsumbua

Meneja wa Msanii mkubwa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale amefunguka na kutaja ugonjwa unaomsumbua Msama Hawa na kudai sio ini kama ilivyoaminika hapo Mwanzoni.

Wiki iliyopita Babu Tale aliondoka na Hawa kwa ajili ya kwenda kufanyiwa matibabu nchini India baada ya Diamond kujitolea msaada wa zaidi ya Milioni 450 kwa ajili ya matibabu yake.

download latest music    

Babu Tale ametoa taarifa kuwa  Hawa atafanyiwa upasuaji wa moyo jioni ya leo Lakini pia Wataalamu wameangalia kila kitu na hawajaona tatizo kwenye Ini kama iliyokuwa inaripotiwa awali.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Babu Tale ameandika:

Asante Mungu tumefika salama India na tumefanya vipimo vyote upya salama na jibu lililotoka kwa wataalamu kwa asilimia 95% awajaona tatizo linalohusiana na ini kwa mgonjwa ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini ivyo basi kutaitajika kufanyika upasuaji mkubwa ambao utakua na uangalizi mkubwa wa wataamu then wametuakikishia baada ya hapo mgonjwa atapata nafuu na inawezekana izo 5% zilizobaki itakua poa na tatizo la ini alitokuwepo kikubwa tunaomba mtuombee dua na msiache kumuombea pia @diamondplatnumz apatenguvu ya kuendela kumsaidia kwa maana kutoa ni moyo. Kikubwa sana naomba tumuombee Hawa coz anaingia kwenye upasuaji mkubwa na hii ni atua ya yeye kua salama. Mungu tusimamie”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.