Bado hali ya Mzee Majuto haijabadilika, adai kuwa anaumwa

Image: Mzee Majuto

Mchekeshaji kutoka Bongo anayetambulika kama King Majuto bado hajapata nafuu hata baada ya kufanyika upasuaji kutokana na tatizo la ugonjwa wa ngiri (hernia).

Hali yake bado haijabadilika kulingana na alichosema baada ya wanahabari kuzungumza naye hivi karibuni. Mzee majuto alisema kuwa bado anahitaji muda mwingi kulala, iliaweze kusikia nafuu.

download latest music    

Baada ya Global publisherz kuzungumza naye, Mzee Majuto alisema:

“Bado nimelala jamani na sijui unataka nini tena? Naumwa na ninasikia maumivu sana na sitaki kuzungumza zaidi maana nimechoka, elewa tu kwamba bado naumwa na ningependa sana uniache ili nipate muda mwingi wa kupumzika, ni kweli hivi karibuni nilipata nafuu kabisa na kuanza kutembea lakini ndiyo hivyo bwana, bado hali haijakaa sawa,”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua