Barakah the Prince afungua YouTube mpya baada ya kuvurugana na lebo linaloongozwa na Alikiba

Alikiba alipandishwa cheo na kuwa mkurugunzi wa label ya RockStar4000 iliyokua imemsimamia Barakah the Prince kabla ya msani huyo kuondoka hivi karibuni.

Barakah The Prince alianza maisha yake mapya akiwa na label yake ya Bana Music baada ya ndoa yake na kampuni ya RockStar4000 kuvunjika.

download latest music    

Staa huyo ametangaza kwa mtandao wa kijamii kuwa anafungua akaunti mpya ya YouTube na kuiacha ile ambayo aliyokuwa akiitumia akiwa katika label ya RockStar4000.

“Ndugu zangu nitawatangazia soon YouTube channel yangu mpya kuna zawadi zenu kama 5 hivi…basi na hii itadondoka ndugu zangu,” aliandika Barakah Instagram.

Hatua hii ya Barakah the Prince imezua madai kuwa RockStar4000 imekataa kupea Barakah akaunti yake ya YouTube ya zamani.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere