Barakah The Prince: Sina Ugomvi Wala Bifu na Alikiba

Mwanamuziki wa Bongo fleva Barakah The Prince ameibuka na kudai kuwa hana ugomvi wala bifu na msanii mwenzake Ali Kiba.

Ni wiki chache tu zilizopita Barakah alikuwa anafanya interview na kila kituo na stesheni mbali mbali za media na kudai kuwa Ali Kiba na uongozi wao wote wa Rockstar 4000 ulikuwa unamfanyia zengwe ili kuua mziki wake baada ya kujitoa kwenye label yao.

download latest music    

Barakah aliyesainiwa chini ya label hiyo ya Rockstar 4000 miaka michache iliyopita aliwashangaza watu wengi kwa kile alichodai kuwa anajitoa kwenye label hiyo kisa na mkasa ukiwa uongozi wa label hiyo ukiongozwa na Ali Kiba na Seven Mosha ulikuwa unamzuia kutoa kazi zake na akadai kuwa kwa mwaka mzima ameruhusiwa kutoa nyimbo moja tu.

Kinachojulikana ni kuwa Ali Kiba alishawahi kusema kuwa Barakah ni mtoto tu hana akili, na inasemekana kuwa aliyemfukuza Barakah Rockstar 4000 ni Ali Kiba kutokana na tabia alizokuwa nazo Barakah. Sasa inasemekana kuwa Barakah ameanza tena kujipendekeza kwa Kiba kwani amemposti Alikiba kwenye siku ya birthday na kumtakia maisha marefu lakini hakumjibu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa Tv kuptia kipindi cha Enews Barakah amedai kuwa hana ugomvi na bifu na Alikiba kama wengi wanavyodhani;

Mimi sijawahi kuwa na matatizo na Alikiba kabisa wala sijawahi kufikiria kuwa na matatizo naye hayo matatizo ni midomo ya watu tu wanayatengeneza, mimi kutaka kuondoka kwenye kampuni yao ya kazi sio kwamba ndio nina ugomvi nao hii ni kazi tu naweza nikahama ofisi yoyote”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.