Barakah The Prince Akubali Msamaha Wa Rommy Jones

Mwanamuziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amekubali msamaha alioombwa na Rommy Jones baada ya kumtongoza mpenzi wake Naj na kisha kumponda Barakah.

Stori hii ilitengeneza headlines wiki iliyopita baada ya meseji za Rommy Jones alizokuwa anamuandikia  Naj kumtongoza kuvujishwa Kwenye mitandao ya kijamii jambo lililozua kizazaa hasa kwa sababu Rommy alikuwa ametoka kuoa na Naj ana mpenzi.

download latest music    

Lakini Kwenye meseji hizo Naj alimkataa Romy na kumwambia anampenda mpenzi wake Barakah lakini cha ajabu alianza kumponda Baraka na kumquat king’asti na pia kusema anazima nyota yake amuache ili akawe mchepuko wake.

Barakah alimjia juu Romy na kuhaidi kumuuliza endapo wakikutana Lakini jana Romy kamuomba msamaha Barakah na bila hiyana Barakah kakubali msamaha Ule na kamtaka wafanye kazi.

Kupitia mtandao wa Instagram Barakah aliandika maneno haya baada ya kuombwa msamaha:

Ni vyema sana Mtu kutambua kosa lake na kutubu..Na anapoomba Msamaha anapaswa kusamehewa..Sina noma na wewe bro,Tupige kazi man”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.