Barnaba Adai Anaogopa Kupiga Picha na Wasichana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Chausiku’ Barnaba Boy amefunguka na kuweka wazi kuwa hivi sasa anahofia sana kupiga picha na wasichana kwa kuhofia uzushi.

Barnaba amefunguka hayo baada ya kuulizwa kuhusu picha zake na wasichana kadhaa ambazo zimekuwa zikionekana Kwenye mitandao ya kijamii na kudaiwa kubadilisha badilisha wasichana.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Barnaba ameweka wazi kuwa wasichana wengine ni mashabiki zake akikutana nao wanaomba picha lakini baadae anasingiziwa ni wanawake wake:

Sio siri siku hizi nimekuwa muoga wa kupiga picha na watoto wa kike na Kuposti Kwenye mitandao ya kijamii naona kama itAleta maneno maneno kuwa ni wapenzi wangu wakati wengi ni mashabiki tu”.

Lakini pia Barnaba alikataa taarifa kuwa tangu ameachana na mama watoto wake MAma Steve amekuwa na wanawake wengi:

Mimi sina mahusiano na wasichana wengi ila nina mashabiki wa kike wengi sana na hata marafiki zangu wengi ni wa kike sio wanaume halafu watoto wa kike wananipenda sana kwa sababu mimi ni mtu ambaye ni mcheshi mtani na mtu wa stori.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.