Barnaba Akiri Ugomvi na Mama Steve Ulishusha Muziki Wake

Msanii wa muziki nchini barnaba classic amefunguka na kusema kuwa moja ya kitu ambacho kimeua sana muziki wake kwa kipindi kifupi cha nyuma ni kutokana na mamatuzo aliyoyapitia hasa kugombana na mama wa mtoto wake.

Hata hivyo, Barnaba anasema kuwa mama steve ni mwanamke aliewahi kuchukua sehemu kubwa sana katika maisha yake lakini kwa sasa anaamini kuwa  kila mtu anatakiwa kuendelea na maisha yake kwa sasa.

download latest music    

Ikumbukwe kuwa siku za hapa karibuni, msanii huyu alisema kuwa siku zote amekuwa akimpenda na hatokaa kumchukia kabisa mama steve kwa sababu ni mama wa mtoto wake na kla siku wataendelea kuwasiliana kwa sababu wana kitu kinawaunganisha  ambacho no mtoto.

Barnaba na mama steve waliweza kukaa katika mahusiano kwa zaidi ya miaka 10 pamoja na kufanikiwa kupata mtoto mmoja , lakini penzi hilo lilikuja kufa mwaka 2018 baada ya mwanadada huyo kuamua kujiingiza katika mahusiano na mwanaume mwingine.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.