Barnaba Amuombea Diamond Msamaha Kwa Zari

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Barnaba Classic ameibuka na kumuangukia Zari kwa magoti na kumuomba asimuache Diamond badala yake Amsamehe.

Siku ya Wapendanao (Valentines Day) Zari alimtosa aliyekuwa Mpenzi wake na Baba wake supastaa wa Bongo fleva Diamond Platnumz baada ya kudai kuwa amechoshwa na skendo zinazotawala kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Tangu tukio hilo litokee watu mbali mbali wamekuwa na cha kusema kuhusu hilo, Barnaba ametumia mtandao wa Instagram kufikisha ujumbe wake kwa Zari na kumuomba afikirie sana uamuzi wake ambapo amemuandikia ujumbe huu:

Zari nahisi maamuzi yako ni magumu sana Mama Tee, people makes mistakes  everyday but hiyo sio sababu ya kumuacha mtu pengine una hasira ila jaribu kufikiria zuri hata moja Diamond alilokufanyia you need more time kufikiria na kufanya maamuzi sahihi tafadhali jamani kuachana sio kuzuri pengine wewe unaweza muacha leo ndio akadumbukia kwenye mikono isiyo salama kwa niaba ya Tanzania tunakuomba Mama Tee msamehe mwenzio japo sijui kosa kubwa ni lipi kalifanya kaka yangu, bado tunahitaji kuona furaha yenu kama wapenzi mlee watoto wenu jamani Happy valentines Chibu family”.

Baada ya maneno hayo aliyoandika mtandaoni kusambaa watu walimgeuka na kumuweka kitimoto kuhusu yeye kuachana na mama watoto wake Mama Steve na kumshauri badala yake apambane na familia yake na achane na familia ya Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.