Barnaba- Mwanamke Anahitaji Kutunzwa Usipofanya Hivyo Wenzako Watakusaidia

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake mpya ya ‘Chausiku’ Barnabas Elias maarufu kama Barnaba Boy Classic ameweka wazi umuhimu wa kumtunza mwanamke.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Wasafi TV, Barnaba amesisitiza matunzo kwa mwanamke ambapo amesema mwanaume kumpatia mwanamke fedha ni sawa na kumwagilia maua.

download latest music    

Nahonga sana kaka na mpaka sasa nahonga, nawachukia wanaume wenzangu wanaosema kuhonga. Mwanamke ukimpa kitu, pesa au talanta yoyote yenye thamani haiitwi kuonga, mwanamke unamzawadia.

Mwanamke ni pambo ambalo linatakiwa kumwagiliwa, ukimpa mpenzi wako pesa umemwagilia ua lako, ume-protect tunda lako, mwanamke anahitaji kutunzwa, usimpomtunza mwenzako watakutunzia”.

Barnaba aliachana na mpenzi wake wa siku nyingi ambaye pia ni mama wa mtoto wake mmoja Steve, Mama Steve Lakini hivi sasa amekuwa akionekana na mwanamke mwingine ambaye ameweka wazi kuwa ni mpenzi wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.