Barnaba- Nikikutana na Vanessa Tunatengeneza Mziki Mzuri

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barnabas Elias ‘Barnaba Boy Classic’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kila akikutana na msanii mwenzake Vanessa Mdee basi wanatengeza hits tu.

Barnaba anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Chausiku’ aliyomshirikisha Vanessa Mdee amedai yeye na Vanessa wana chemistry fulani Inayovutana mpaka kutengeneza nyimbo kali.

download latest music    

Barnaba alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, amedai kuwa mashabiki zao wenyewe wanafahamu wakikutana yeye na Vanessa nini kitatokea ndio maana wanafanya vizuri:

Mashabiki wanajua mimi nikikutana na Vanessa kuna mambo mazuri yanakuja, sisi tuna chemistry ya pamoja, sauti zetu zimekuwa zikikutana pamoja kuna mambo mazuri yanatokea”.

Lakini pia Barnaba ameweka wazi kuwa kwa sasa mashabiki wameshachoshwa na kelele wanataka mziki mzuri:

Hii inaonyesha kazi ni nzuri watu wanapenda muziki mzuri, watu wamechoshwa na makelele wanahitaji muziki mzuri, na ukweli kazi na sio maneno maneno”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.