Beka Flavour: Mimi ndiyo Justine Beiber wa Bongo

Msanii aliyekuwa katika kundi ya Yamoto Band – Beka Flavour amefunguka na kusema kuwa yeye ndo Justine Beiber wa Bongo.

Akiongea na E-Newz ya EATV, Beka alisema kuwa yeye sasa ameachana na mambo ya kiki kwasababu anataka kuboresha muziki wake.

download latest music    

“Siku hizi hamna muziki wa maneno mengi na kiki sema mimi nilikuwa naona vile vitu vilikuwa vinaendelea mtandaoni. Ukweli hamna kitu kama hicho mimi nafanya muziki wangu binafsi halafu ninaamini ni wakwangu, mimi ndiyo Justine Beiber wa Bongo,” amesema Beka Flavour.

Beka Flavour

Staa huyo pia aliwakashifu wanahabari kwa kumliganisha na Aslay ambaye alikuwa naye Yamoto Band. Beka alisema kuwa yeye hafanyi muziki ya ushindani na kuongeza kuwa hana tatizo na msanii wowote wa Bongo.

“Wanatakiwa watusapoti, siyo poa wanavyoandika wanatushindanisha halafu mimi sifanyi muziki wa ushindani na miaka 100 siwezi nikafanya muziki wa ushindani sina tatizo na msanii yeyote kutoka Tanzania.”

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere