Bella Adaiwa Kutelekeza Kichanga Chake na Kwenda Kula Bata Zenji

Msanii wa filamu za Bongo Movie Isabella Mpanda maarufu kama Bella amekumbwa na skendo ya kumtelekeza mtoto wake mchanga aliyejifungua Miezi michache iliyopita na kutimkia Zenji kula raha.

Global Publishers wanaripoti kuwa Bella  anadaiwa kuacha kichanga cha miezi mitatu na kwenda kula bata visiwani Zanzibar au Zenji ambapo inadaiwa Bella alinaswa kwenye hoteli moja visiwani humo iliyojulikana kwa jina la Coral Beach akiwa na mlezi wa Bongo Muvi, Catherine Ambakyise ‘Mama Lola’ wakila bata la hatari.

download latest music    

Chanzo ambacho ni rafiki wa karibu wa Bella kimeiambia Ijumaa Wikienda kwamba, hata marafiki zake  wanamshangaa mno shoga yao huyo kwa kitendo alichokifanya cha kumwacha mtoto wake huyo mdogo na kwenda kula bata.

Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilimsaka Bella ili kupata ukweli wa tuhuma hizo nzito ambapo ambapo mwenyewe alifunguka:

Mimi naomba, sitaki kuzungumza hilo, wewe jua tu mwanangu yupo sehemu salama, hana shida yoyote na ninakuomba sana, sitaki habari hii itoke gazetini kwa sababu sijawahi kukunyima ushirikiano“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.