Belle 9- Siuelewi Kabisa Muziki wa Madee

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva aliyetamba na kibao chake cha ‘Masogange’ Belle 9 amefunguka na kumrushia Dongo Zito msanii mwenzake Madee Ali Raisi wa Manzese.

Belle ameweka wazi kuwa Madee ni mmoja kati ya wasanii wa Bong fleva ambaye haelewi muziki wake anaoufanya.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na  JJ wa Jembe FM, Belle 9 amesema kuwa kutokana anasikiliza wachanaji wengi wanaofanya vizuri anahisi kuna kitu anakikosa kutoka kwa Madee.

Honesty, let me be honesty, Madee huwa simuelewi. I don’t know, ujue kuna wasanii inafika kipindi unasikiliza unasema huyo mtu ana-release beat sio wimbo tena.

Labda kwa vile nasikiliza rappers ambao wanajua sana au kuna kitu nakitegemea kutoka kwake kutokana muda mrefu yupo kwenye game, kuna kitu nakimisi, so naona kama nikimsiliza na lose”.

Baada ya kimya cha muda mrefu Belle 9 amerudi kwa kasi ya ajabu ambapo kibao kipya cha ‘Dada‘ kimeendelea kufanya vizuri katika vituo mbali mbali vya habari Lakini pia hata mitandao ya kijamii kama Youtube ambapo umeshika nafasi za juu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.