Ben Pol amjibu mchekeshaji aliyelia na kumwomba amuoe

Mchekeshaji wa kike Ebitoke anampenda Pel Pol kwa dhati, alilia akifanya mahojiano huku akimwomba Ben Pol amuoe.

Ebitoke alifungua roho katika mahojiano na Sasa TV na kueleza jinsi anavyompenda Ben Pol, alisema ishu ya Ben Pol kuwa na mtoto ilimuuma sana kwasababu alikua anadhani ako na bibi.

download latest music    

https://www.youtube.com/watch?v=h_cKUc2TVgQ

Ben Pol amemjibu Ebitoke, anataka kukutane naye uso kwa uso ili kudhibitisha kama mchekeshaji huyo anamaanisha anachosema ama ni utani tu.

“Kwanza niseme tuu naheshimu hisia za kila mtu yeye ni binadamu na ameonesha hisia zake soo naziheshimu sana. Kweli nimeziona habari mitandaoni tuu tangia jana watu wakiposti lakini sikuamini siunajua habari za mitandao bro! ila leo pia nimeona video yake akisisitiza ombi lake lakini bado siamini na nitaamini na nitafurahi kama tukionana uso kwa uso,” alisema Ben Pol.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere