Ben Pol Arudisha Mapigo Kwa TID na Kudai Amemkosea Heshima

Wasanii wa mziki wa Bongo fleva TID mnyama na Ben Pol wamejikuta kwenye bifu zito baada ya TID kumtolea povu zito Ben Pol baada ya kuimba nyimbo yake kwenye tamasha la Fiesta lililofanyika wikiend iliyopita.

TID alimjia juu Ben Pol baada ya kuimba kiitikio cha wimbo wake wa ‘Nyota yangu’ katika tamasha la Fiesta bila ruhusa yake ambapo TID alikiambia kituoa cha redio cha East Africa kuwa ana mpango wa kuzungumza na wakubwa wake pamoja na wanasheria ili kumchukulia Ben Pol hatua za kisheria kwa kuiba nyimbo yake.

download latest music    

Kwenye mahohiano aliyofanya na Bongo 5, Ben Pol amemtaka msanii huyo mkongwe kumuomba radhi kwa kauli yake aliyoitoa:

Unajua kilichotokea ni kwamba wimbo wangu wa moyo mashine unaendana na nyota yangu kwa sababu zote zina miondoko ya Zhouk kwaiyo yaani pale nilikuwa kama nampa heshima fulani hivi yeye na mziki wake. Kwanza kiukweli kabisa TID ni msanii aliyeni-insipire mimi mpaka nikaanza kuimba mimi nipo shule ya msingi nasikiliza albamu ya sauti ya dhahabu naiimba yote yaani pale ndipo Ben Pol alipozaliwa kwaiyo nilishangaa yeye kuwaka mimi kuimba kionjo cha nyimbo yake wakati yeye ni staa na ni msomi kama nsanii anaelewa hizo mambo zipo lakini sikutegemea msanii mwenye heshima yake Kama yete anaweza kufanya kitu kama mile kusema kweli I am very confused”.

Lakini pia Ben Pol amekiri kuwa hawezi kumlaumu sana TID kwani hawezi jua wakati anafanyaile interview alikuwa katika hali gani na anaamini akikaa akitulia amtafute Ben Pol amuombe  radhi kwa kitendo alichofanya kwani yeye anajua hakikuwa sawa kabisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.