Bifu ya wasanii wakongwe: Q Chief amchana TID

Q Chief anadai kuwa msanii mwenzake mkongwe – TID ako na matatizo ya kisaikolojia. Chief amesema haya baada ya kugadabishwa na tabia ya TID.

Akiongea na Times FM, Q Chief alieleza kuwa chanzo cha bifu yake na TID ni tabia ya msanii huyo kufwatilia maisha ya watu wengine huku akiacha kupambana na hali yake.

download latest music    
Q Chief

Chief alimshauri TID kuwa ni bora angejitahidi kuangalia jinsi ya kurudi kwenye muziki badala ya kujishugulisha kuzungumzia vitu visivyomuhusu.

“Mimi naona kama watu wazima kila mtu angelia na hali yake na kuangalia jinsi gani anaweza kurudi kwenye sehemu yake, Kwahiyo mimi huwa nachukulia kwanini niwe tatizo kwa mtu mwingine? nahisi kuna kitu special umekiona kwangu na hutaki kuniambia utakuwa unamatatizo. TID anamatatizo ya kisaikolojia hivyo anatakiwa ajitathmini kiundani, kama mpaka waheshimiwa wameamua kukusaidia lazima uoneshe muelekeo ili waendelee kukusaidia,” amesema Q Chief

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere