Caroline Joseph Amefunguka Kuhusu Tetesi Za Ujauzito Wa Alikiba

Mwanadada Caroline Joseph ameongelea tetesi zilizomkabili mtandaoni kuhusu yeye kutangaza kuwa ana ujauzito wa mwanamuziki Ali Saleh kiba.

Ni wiki chache tu zimepita tangu mwanamuziki Ali Kiba akumbwe na skendo ya picha zilizosambaa mtandaoni zinazomuonesha yeye na mwanadada Caroline wakiwa chumbani wamepiga picha pamoja, lakini haraka sana msemaji wa Kiba aliibuka na kusema Kiba hana uhusiano wowote na yule dada ila tu nishabiki aliyemfata kupiga picha kama walivyo mashabiki wengine.

download latest music    

Wiki iliyopita kuna picha ya ‘Ultrasound’ ya mtoto iliyodaiwa kuwekwa na Caroline mtandaoni akidai kuwa anatarajia kujifungua mtoto wa kike wa Kiba.

Picha iliyodaiwa kupostiwa na Caroline akidai ni ultrasound ya ujauzito wake

Caroline amefunguka kuhusu sakata hilo lililokiki mtandaoni amesema ameshtushwa na habari hizo zilizosambaa kwani sio za kweli na anamheshimu Kiba kama kaka na ndugu yake.

Sina mimba jamani na wala sina uhusiano na Kiba, kuna mtu amefungua akaunti feki kwa kutumia jina langu kwenye mtandao wa Instagram Ambaye anasema ana ujauzito wa Kiba na ameweka picha zangu eti na ultrasound ya mtoto tumboni na kusema Princess Kiba anakuja! Kiukweli imeniuma sana maana imenipa usumbufu hivyo nimeenda kuripoti polisi katika kitengo cha makosa ya kimtandao (cyber crimes)na wako kwenye uchunguzi wa kumpata huyo mtu aliyetumia jina langu na kuweka picha zangu kunichafua ili achukuliwe hatua”.

Pia, Caroline aliweka wazi kuwa amekuwa akipokea meseji za vitisho kwenye simu yake kwa namba ngeni Kwamba watamfanyia kitu kibaya kwa kuwa anamchafua Kiba kwa kusema ana mimba yake.

Nimepokea vitisho kwenye Simu yangu kuwa watanipoteza kwasababu namchafua Alikiba lakini nimekuwa nikiwaambia waangalie kwenye Instagram mimi natumia jina la Dorothea Caroline 9, huyo aliyeweka hiyo picha Hana 9 mwishoni. Nimeamua kwenda polisi ili huyo mtu akamatwe maana naweza kupatwa na jambo baya Wakati sina hatia yoyote Huyo mtu inawezekana anatafuta wafuasi kwaajili ya kufanya biashara zake”.

Ali Kiba alikataa kujibu tuhuma hizo hata kupitua meneja wake alipotafutwa alikataa kuongelea suala hill.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.