Chid Benz Amwaga Povu Baada Ya Kukosekana Kwenye Listi Ya Wasafi Festival

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop nchini Chid Benz amefunguka na kuwamwagia Povu zito timu nzima ya WCB Baada ya kukosa mwaliko wa kufanya shoo kwenye Wasafi Festival.

Chid Benz amefungukia ishu ya Diamond Platnumz na Timu yake nzima ya WCB kutumia wanamuziki Kama Dudubaya ambaye anaamini amechaguliwa kwa sababu ya umaarufu wa jina lake Konki Konki konki Master.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, Chid Benz amedai amesikiyishwa kuwa Msanii Kama yeye Anayeimba vitu vya maana hajachaguliwa kwa madai kuwa anatumia madawa ya kulevya ilhali ameshaacha.

Sisi wasanii tunaoimba nyimbo ambazo zinabeba ujumbe na maana hatupati nafasi kabisa utasikia wanasema achana na hao wakina Chidi Benz wanakula unga ila Dudubaya kisa anasema konki konki anajaza watu basi nasibu anampa tour kwenye Wasafi Festival”.

Diamond na timu nzima ya WCB ilimchagua Dudubaya Kama mmoja wa wasanii watakaoshiriki katika tamasha la WCB Baada ya umaarufu alioupata kupitia jina lake la utani la Konki Master.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.