Chidi Benz akamatwa baada ya kunaswa na Heroine

Chidi Benz ambaye alikuwa ameachia wimbo mpya unaofahamika Kama ‘Muda’ aliyomshirikisha Q Chillah amjipata mashakani baada ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya heroine.

Kulingana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alifunguka kusema kuwa Chid Benz alipatikana baada ya msako na mkali uliofanyika August 12 jioni.

download latest music    

“Chid Benz na wenzake wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”

Chid Benz ambaye ambaye alikuwa anaonekana kubadilika amewashtua wengi kwani hii sio mara yake ya kwanza kupatikana na Sawa za kulevya.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua