Christian Bella Amefungukia Ishu Ya Hamisa na Diamond

Mwanamuziki maarufu wa dansi, Christian Bella ameongelea habari ambayo bado inashika vichwa vya habari, uhusiano kati ya Hamisa Mobetto na mzazi mwenziye Diamond Platnumz.

Christian Bella aliyetumbuiza kwenye sherehe ya mtoto wa Hamisa, Kwenye mahojiano na Bongo 5 Bella ameongelea mawazo yake juu ya kinachoendelea kati ya Diamond na Hamisa:

download latest music    

Hamisa kwangu mimi ni mwanadada anayejituma ni model si unaona mpaka anapata tunzo za nje ya nchi, mi namuona ni mtu mzuri tu ambaye hana tatizo na piano suala la Hamisa na diamond kupelekana mahakamani mi sidhani kama Diamond anaweza kushindwa au anaweza kukataa kumlea mtoto wake ilimradi ameshakubali kuwa mtoto ni wa kwake”.

Pia Christian Bella hakuishia hapo aliendelea kuweka maneno:

Mi naona umefika wakati wawili hawa wakae chini wayaongee tu kistaarabu kwani Naseeb hawezi akashindwa au akamletea roho mbaya kwa sababu yule ni mtoto wake alafu isitoshe Naseeb mwenyewe kapitia maisha magumu kakulia Tandale kwaiyo anaelewa ugumu na Kama kweli hajatoa mi naaminmawa na misunderstanding hivyo wakae wayaongee mi naamini hapatatokea makelele yoyote”.

Kuhusu suala la kupelekana mahakamani Hamisa alielezea kuwa Diamond ndio aliyetaka iwe vile, yaani atafute mwanasheria na afungue kesi mahakamani ili wapate mwongozo wa kisheria wa jinsi Diamond ataweza kumtunza mtoto bila tatizo lolote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.