Chuchu Hansy Akana Mahusiano na Frank Baada Ya Kumwagana na Ray

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy ambaye pia ni mzazi mwenzake na staa mkongwe Vicent Kigosi ‘Ray’ amekana kuwa kwenye mahusiano na Msanii mwingine Frank Mtao.

Wiki chache zilizopita Chuchu Hansy na Ray waliweka wazi kuwa baada ya mahusiano ya miaka mingi na Mtoto mmoja wameamua kutengana. Lakini muda mfupi Kupita kumekuwa na tetesi Chuchu Hansy yupo kwenye mahusiano na Frank.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya Gazeti la  Ijumaa Wik­ienda, Chuchu alisema anachojua Frank ni mzazi mwenziye na walishamalizana muda mrefu kili­chobaki kati yake na yeye ni mtoto na si kitu kingine.

Unajua nashangaa hata hayo madai ya Frank na mimi yameibu­kia wapi kwa sababu yule mtu ana familia yake na mimi nina maisha yangu mengine kabisa, sijui kwa nini watu wanapenda kuingilia familia za watu, yule na mimi imebaki stori na ni kwa sababu ya mtoto“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.