Chuchu Hansy- Siwezi Kumchukia Ray

Msanii wa Bongo movie Chuchu Hansy amefunguka na kusema kuwa hawezi kumchukia msanii mwenzake Vicent Kigosi ‘Ray’ ambaye ni baba wa Mtoto wake.

Kwa Wiki kadhaa sasa kumekuwa na tetesi kuwa penzi la Ray na Chuchu Hansy limefika mwisho Baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa miaka mingi na kuzaa pamoja Mtoto mmoja.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Enews cha EATV, Chuchu amesema kuwa hawezi kumchukia Ray hata siku moja kwa sababu atabaki kuwa baba wa Watoto Wake hata kama wakiachana au wakiendelea kuwa wote.

Siwezi kabisa kuongelea mahusiano yangu na Ray kwa sababu hayo ni maisha yangu binafsi Lakini mimi na yeye tupo sawa kwa sababu tunalea mtoto kwa pamoja hivyo hamna shida”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.