Darassa Ajibu Tuhuma Za Kutumia Madawa Ya Kulevya

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye aliwahi kujizolea umaarufu na kibao chake cha ‘Muziki’ Darassa CMG ameibuka baada ya kimya kirefu na kukiri tuhuma zilizowahi kumkabili za kutumia madawa ya kulevya.

Miaka michache iliyopita Darassa alitoa bonge la ngoma lakini Baada ya mafanikio hayo alikuwa kimya kiasi cha kupelekea maneno kusambaaa kuwa msanii huyo amejitumbukiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya Gazeti la Risasi Jumamosi, Darassa alisema kuwa mara baada ya kuachia Muziki aliamua kukaa kimya kwa ajili ya kuwa karibu na familia baada ya kupata mtoto wa kike.

Watu walikuwa wakiongea wanayojua wao. Ukweli nipo fiti, sijawahi kujihusisha na vitu kama hivyo. Ukimya wangu sasa hivi umefika mwisho na nimerudi rasmi”.

Darassa amekiri tetesi za madawa zilikuwa zinamuumiza sana ingawaje alikuwa Anajua kuwa hazina ukweli wowote.

Hivi sasa Darassa anafanya vyema na ngoma yake ya ‘Achia njia’ ambayo imeshika nafasi za juu katika chati za YouTube.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.