Davina Aamua Kupita Barabara ya Shiloleh

Mwanadada kutoka tasnia ya bongo movies, Davina amefunguka na kusema kuwa kwa sasa hivi ni wasanii na wanawake wachache sana wanaoshinda masaluni kwa ajili ya kukaa na kutengeneza kucha kwa sababu wanakuwa na mambo mengi ya kufanya na haina haja ya kuwa na urembo usiokuwa na faida.

Davina ambae kwa sasa amekiri kujiingiza katika swala la ujasiriamali wa muda mrefu kidogo huku akihuska na kupika chakula ambacho wateja wake wakubwa ni wanafunzi kutoka chuo cha UDSM.

download latest music    

Sidhani kama kuna msanii anaewaza sasa hivi kwenda kukaa saluni kwa ajili ya kutengeneza au kuosha kucha zake kama ilivyokuwa huko nyuma, siku hizi mimi na jiko na jiko na mimi tu.

Wasanii wengi wa kike kutoka bongo movies kwa sasa wamekuwa wakijitahidi kutumia majina yao na vipaji walivyonavyo kwa ajili ya kujiingiza katika ujasiriamali na kupata pesa kwa njia nyingine tofauti na uigizaji.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.