Diamond Abadili Tarehe Ya Ndoa Yake na Tanasha

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz amesogeza mbele tarehe ya ndoa yake na Mpenzi Wake Mkenya Tanasha Donna.

Siku chache Baada ya kuweka hadharani mapenzi yake Man mrembo Tanasha Diamond alitangaza nia yake ya kumuoa binti huyo na kusema ndoa yao ingekuwa tarehe 14 mwezi wa pili siku ya Wapendanao duniani.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha Wasafi Tv, Diamond amesema kuwa tarehe waliyopanga awali kwa ajili ya ndoa wameisogeza mbele kutokana anataka harusi yake iwe nzuri na kuhudhuriwa na watu wengi.

Ndoa yangu ilitakiwa iwe siku ya Valentine tarehe 14 lakini tumeipeleka mbele. Watu wengi wanatakiwa kuja kuhudhuria kwa sababu ndoa yangu watakuja kina Rick Ross”.

Mara ya kwanza Diamond alipotangaza kumuoa Tanasha Siku ya wapendanao mwaka huu ilivutia watu wengi kwani siku ya wapendanao mwaka jana Diamond aliingia kwenye headlines baada ya aliyekuwa Mpenzi Wake Zari kumtosa kwa ya Jeusi Kupitia ukurasa wake wa Instagram.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.