Diamond afunguka sababu maalum ya kuwasilisha Young Killer kwenye wimbo wake mpya

Watu wengi ikiwemo wana WCB walishangazwa sana na uamuzi wa Diamond kumwasilisha Young Killer katika wimbo wake mpya.

Na kwa sababu gani?

download latest music    

Diamond alifunguka kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM na kusema hivi:

”Nilimuita Young Killer kuja studio, nikamwambia sijawahi kumshirikisha mtu katika muziki kipindi hiki na nikimshirikisha mtu ni wa WCB, kuna nyimbo yangu nataka nikushirikishe tufanye. Kwanza alipata shock kidogo, alipagawa kidogo”

“Nikamwambia usipagawe, hii nyimbo ukifanya verse mbovu nakufuta na hapa katika ofisi mimi ndio nimekupigania hili swala uingize verse kwa sababu kila mtu anashangaa kwanini Young Killer? Ile verse imeandikwa ndani ya siku hizi tatu, akanambia hii nyimbo angekuwa mtu mwingine ningeshamaliza. Katika intro ya kutafuta kuingilia alitafuta karibuni hata masaa sita, lakini mwisho wa siku amefanya verse kali sana sana, imeshaisha bado kushoot video ngoma itoke,” ameongeza.

Bosi huyo wa WCB amesisitiza, “Young Killer mtu ambaye masikini ya Mungu anajitahidi sana sana kufight na mtu ambaye anaandika, mimi napenda mtu anavyandika. Nikajua kwanza nikimchukua Young Killer, nitawaempower vijana wengine wengi wenye ndoto ya kufanya muziki kuona kwamba kumbe na sisi tunawezekana. Kwasababu wangejua Diamond angefanya ngoma labda na Fid Q na Joh, wao wanajua hizo ndio atafanya nao, lakini nimeonyesha kuwa yoyote ninaweza nikafanya naye nyimbo. Na Young Killer kiukweli anachokifanya ni kitu kikubwa na video tutashoot hapa hapa Tanzania na ngoma ni kali na yakinyamwezi.”

About this writer:

Irari Ngugi

Lover of life, lover of big boobs and certified celebrity squasher. Catch me if you can on facebook as Irari Ngugi