Diamond Amkabidhi Mpiga Picha Wake Gari Jipyaa

Msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemfanyia bonge la surprise mpiga picha wake anayejulikana kama Lukamba baada ya kumkabudhi gari jipya.

Diamond amempa gari aina ya Toyota Alteza Lukamba siku ya Ijumaa iliyopita alipoenda kutoa msaada Tandale, ambapo Diamond alifunguka:

download latest music    

Lukamba anakaa Bunju, kuna kipindi alikabwa na kuchukuliwa hadi laptop sasa leo nampatia gari,”

Baada ya kukabidhiwa gari hilo, Lukamba alimuandikia Diamond ujumbe huu Kupitia ukurasa wake wa Instagram:

Hadi Sasa Nimekosa Maneno Ya Kuandika Yatakayoweza Kubeba Hisia Zangu Za Furaha Niliyonayo,Nimekuwa Nikiandika Na Kufuta Kila Neno Ninaloandika Naona Halijitoshelezi Nahisi Halina Uzito Kuelezea Kilichopo Moyoni Mwangu….. Bro @diamondplatnumz umekuwa msaada sana kwa Sisi vijana maskini wenzako, Mungu azidi kukupa moyo wa kidogo unachopata kugawana na wenzako, pia nishkuru uongozi wa @wcb_wasafikwa kudhamini kidogo changu hii imenipa moyo sana wa kuzidi kujituma zaidi na zaidi
God bless you simbaaa ????????????@diamondplatnumz”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.